Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
37.Suurat Ass 'Affat

Imeshuka Makka Ina aya 182
Utangulizi Sura Nyingine Faharasa


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0



1. Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. 1



2. Na kwa wenye kukataza mabaya. 2



3. Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. 3



4. Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. 4



5. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote. 5



6. Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota. 6



7. Na kulinda na kila shet'ani a'si. 7



8. Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande. 8



9. Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu. 9



10. Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara. 10



11. Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata. 11



12. Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. 12



13. Na wanapo kumbushwa hawakumbuki. 13



14. Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara. 14



15. Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri. 15



16. Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa? 16



17. Hata baba zetu wa zamani? 17



18. Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili. 18



19. Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona! 19



20. Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo. 20



21. Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha. 21



22. Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu. 22



23. Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu! 23



24. Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa: 24



25. Mna nini? Mbona hamsaidiani? 25



26. Bali hii leo, watasalimu amri. 26



27. Watakabiliana wao kwa wao kuulizana. 27



28. Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia. 28



29. Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini. 29



30. Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu. 30



31. Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. 31



32. Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu. 32



33. Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja. 33



34. Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu. 34



35. Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna. 35



36. Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? 36



37. Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume. 37



38. Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu. 38



39. Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya. 39



40. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. 40



41. Hao ndio watakao pata riziki maalumu, 41



42. Matunda, nao watahishimiwa. 42



43. Katika Bustani za neema. 43



44. Wako juu ya viti wamekabiliana. 44



45. Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem. 45



46. Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao. 46



47. Hakina madhara, wala hakiwaleweshi. 47



48. Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri. 48



49. Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. 49



50. Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe. 50



51. Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki. 51



52. Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki. 52



53. Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa? 53



54. Atasema: Je! Nyie mnawaona? 54



55. Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu. 55



56. Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza. 56



57. Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. 57



58. Je! Sisi hatutakufa, 58



59. Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa. 59



60. Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa. 60



61. Kwa mfano wa haya nawatende watendao. 61



62. Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum? 62



63. Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu. 63



64. Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu. 64



65. Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani. 65



66. Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo. 66



67. Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka. 67



68. Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu. 68



69. Hakika waliwakuta baba zao wamepotea. 69



70. Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. 70



71. Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. 71



72. Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. 72



73. Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. 73



74. Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. 74



75. Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji. 75



76. Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa. 76



77. Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia. 77



78. Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye. 78



79. Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote! 79



80. Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. 80



81. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. 81



82. Kisha tukawazamisha wale wengine. 82



83. Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake, 83



84. Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima. 84



85. Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini? 85



86. Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu? 86



87. Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote? 87



88. Kisha akapiga jicho kutazama nyota. 88



89. Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! 89



90. Nao wakamwacha, wakampa kisogo. 90



91. Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli? 91



92. Mna nini hata hamsemi? 92



93. Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia. 93



94. Basi wakamjia upesi upesi. 94



95. Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe 95



96. ?Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! 96



97. Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo! 97



98. Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini. 98



99. Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. 99



100. Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema. 100



101. Basi tukambashiria mwana aliye mpole. 101



102. Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri. 102



103. Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji. 103



104. Tulimwita: Ewe Ibrahim! 104



105. Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema. 105



106. Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri. 106



107. Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. 107



108. Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye. 108



109. Iwe salama kwa Ibrahim! 109



110. Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. 10



111. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. 11



112. Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema. 112



113. Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi. 113



114. Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni. 114



115. Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa. 115



116. Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda. 116



117. Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha. 117



118. Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. 118



119. Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. 119



120. Iwe salama kwa Musa na Haruni! 120



121. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. 121



122. Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini. 122



123. Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume. 123



124. Alipo waambia watu wake: Hamwogopi? 124



125. Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji, 125



126. Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani? 126



127. Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa; 127



128. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. 128



129. Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye. 129



130. Iwe salama kwa Ilyas. 130



131. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. 131



132. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. 132



133. Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. 133



134. Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote, 134



135. Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma. 135



136. Kisha tukawaangamiza wale wengineo. 136



137. Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi, 137



138. Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini? 138



139. Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume. 139



140. Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni. 140



141. Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa. 141



142. Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. 142



143. Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu, 143



144. Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa. 144



145. Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa. 145



146. Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye. 146



147. Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi. 147



148. Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda. 148



149. Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume? 149



150. Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia? 150



151. Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema: 151



152. Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo! 152



153. Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume? 153



154. Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi? 154



155. Hamkumbuki? 155



156. Au mnayo hoja iliyo wazi? 156



157. Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli. 157



158. Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa. 158



159. Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia. 159



160. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. 160



161. Basi hakika nyinyi na mnao waabudu 161



162. Hamwezi kuwapoteza. 162



163. Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni. 163



164. Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu. 164



165. Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. 165



166. Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa. 166



167. Na walikuwapo walio kuwa wakisema: 167



168. Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani, 168



169. Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi. 169



170. Lakini waliukataa. Basi watakuja jua. 170



171. Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa. 171



172. Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa. 172



173. Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda. 173



174. Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda. 174



175. Na watazame, nao wataona. 175



176. Je! Wanaihimiza adhabu yetu? 176



177. Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa. 177



178. Na waache kwa muda. 178



179. Na tazama, na wao wataona. 179



180. Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia. 180



181. Na Salamu juu ya Mitume. 181



182. Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. 182


Sura Nyingine Faharasa
Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani