63.Suuratul Al Munaafiqun |
Imeshuka Madina | Ina aya 11 |
Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0
1. Wanapo kujia wanaafiki husema: Tunashuhudia ya kuwa wewe ni Mtume
wa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi
Mungu, na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa hakika wanaafiki ni waongo.
1
2. Wamevifanya viapo vyao ni kinga, na wao wakajizuia kuifuata Njia
ya Mwenyezi Mungu. Hakika ni mabaya kabisa waliyo kuwa wakiyafanya.
2
3. Hayo ni kwa sababu ya kuwa waliamini, kisha wakakufuru; kwa hivyo
umepigwa muhuri juu ya nyoyo zao. Kwa hivyo hawafahamu lolote.
3
4. Na unapo waona, miili yao inakupendeza, na wakisema, unasikiliza
usemi wao. Lakini wao ni kama magogo yaliyo egemezwa. Wao hudhania kila
ukelele unao pigwa ni kwa ajili yao. Hao ni maadui; tahadhari nao. Mwenyezi
Mungu awaangamizilie mbali! Vipi wanapotoka na haki?
4
5. Na wanapo ambiwa: Njooni ili Mtume wa Mwenyezi Mungu akuombeeni
maghfira, huvigeuza vichwa vyao, na unawaona wanageuka nao wamejaa kiburi.
5
6. Sawa sawa kwao, ukiwatakia maghfira au hukuwatakia maghfira, Mwenyezi
Mungu hatawaghufiria. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wapotovu.
6
7. Hao ndio wanao sema: Msitoe mali kwa ajili ya walioko kwa Mtume
wa Mwenyezi Mungu, ili waondokelee mbali! Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye
khazina za mbingu na ardhi, lakini wanaafiki hawafahamu.
7
8. Wanasema: Tukirejea Madina mwenye utukufu zaidi bila ya shaka
atamfukuza aliye mnyonge. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye utukufu - Yeye,
na Mtume wake, na Waumini. Lakini wanaafiki hawajui.
8
9. Enyi mlio amini! Yasikusahaulisheni mali yenu, wala watoto wenu,
kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Na wenye kufanya hayo ndio walio khasiri.
9
10. Na toeni katika tulicho kupeni kabla hayajamfikia mmoja wenu
mauti, tena hapo akasema: Mola wangu Mlezi! Huniakhirishi muda kidogo nipate
kutoa sadaka, na niwe katika watu wema?
10
11. Wala Mwenyezi Mungu hataiakhirisha nafsi yoyote inapo fika ajali
yake; na Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda.
11
Sura Nyingine | Faharasa |