Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
99.Surat Az-Zilzalah

Imeshuka Madina Ina aya 8
Utangulizi Sura Nyingine Faharasa


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0



1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! 1



2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake! 2



3. Na mtu akasema: Ina nini? 3



4. Siku hiyo itahadithia khabari zake. 4



5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!



6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! 6



7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! 7



8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! 8


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani