101.Surat Al-Qaaria'h |
Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
Utangulizi | Orodha ya Sura |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0
1. Inayo gonga! 1 2. Nini Inayo gonga? 2 3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? 3 4. Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; 4 5. Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! 5 6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, 6 7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. 7 8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, 8 9. Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! 9 10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? 10 11. Ni Moto mkali! 11
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani |