Adh Dhuhaa Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
93.Surat Wadh-Dhuhaa

Imeshuka Makka Ina aya 11
Utangulizi Orodha ya Sura Faharasa

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0


1. Naapa kwa mchana! 1


2. Na kwa usiku unapo tanda! 2


3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe. 3


4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. 4


5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. 5


6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? 6


7. Na akakukuta umepotea akakuongoa? 1


8. Akakukuta mhitaji akakutosheleza? 8


9. Basi yatima usimwonee! 9


10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! 10


11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. 11


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani