95.Surat At-Tin |
Imeshuka Makka | Ina aya 8 |
Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0
1. Naapa kwa tini na zaituni! 1
2. Na kwa Mlima wa Sinai! 2
3. Na kwa mji huu wenye amani! 3
4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. 4
5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini! 5
6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. 6
7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? 7
8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote? 8
Sura Nyingine | Faharasa |