Al Zilzalah Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
99.Surat Az-Zilzalah

Imeshuka Madina Ina aya 8
Utangulizi Sura Nyingine Faharasa

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0


1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! 1


2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake! 2


3. Na mtu akasema: Ina nini? 3


4. Siku hiyo itahadithia khabari zake. 4


5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!


6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! 6


7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! 7


8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! 8


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani