100.Surat Al-A'adiyaat |
Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0
1. Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua, 1
2. Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini, 2
3. Wakishambulia wakati wa asubuhi, 3
4. Huku wakitimua vumbi, 4
5. Na wakijitoma kati ya kundi, 5
6. Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi! 6
7. Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo! 7
8. Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali! 8
9. Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini? 9
10. Na yakakusanywa yaliomo vifuani? 10
11. Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote! 11
Sura Nyingine | Faharasa |