105.Surat Al-Fiil |
Imeshuka Makka | Ina aya 5 |
Utangulizi | Sura Nyingine | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0
1. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? 1
2. Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? 2
3. Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, 3
4. Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, 4
5. Akawafanya kama majani yaliyo liwa! 5
Sura Nyingine | Faharasa |