Ash-Shu'araa Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
26.Suurat Shu'araa

Imeshuka Makka Ina aya 227
Utangulizi Sura Nyingine Faharasa

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0


1. T'aa Siin Miim. (T'.S.M.) 1


2. Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha. 2


3. Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini. 3


4. Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao. 4


5. Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao. 5


6. Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha. 6


7. Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri? 7


8. Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini. 8


9. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 9


10. Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu, 10


11. Watu wa Firauni. Hawaogopi? 11


12. Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe. 12


13. Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun. 13


14. Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa. 14


15. Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza. 15


16. Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 16


17. Waachilie Wana wa Israili wende nasi. 17


18. (Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi? 18


19. Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani? 19


20. (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea. 20


21. (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea. 21


22. Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili? 22


23. Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote? 23


24. Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini. 24


25. (Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi? 25


26. (Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza. 26


27. (Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu. 27


1 28. (Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini. 28


29. (Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani. 29


30. Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi? 30


31. Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli. 31


32. Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri. 32


33. Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao. 33


34. (Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu. 34


35. Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani? 35


36. Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo. 36


37. Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu. 37


38. Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu. 38


39. Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika? 39


40. Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda. 40


41. Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda? 41


42. Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele. 42


43. Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa. 43


44. Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda. 44


45. Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua. 45


46. Hapo wachawi walipinduka wakasujudu. 46


47. Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote. 47


48. Mola Mlezi wa Musa na Harun. 48


49. (Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote. 49


50. Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi. 50


51. Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini. 51


52. Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa. 52


53. Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo. 53


54. (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo. 54


55. Nao wanatuudhi. 55


56. Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari. 56


57. Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem, 57


58. Na makhazina, na vyeo vya hishima, 58


59. Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili. 59


60. Basi wakawafuata lilipo chomoza jua. 60


61. Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana! 61


62. (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa! 62


63. Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa. 63


64. Na tukawajongeza hapo wale wengine. 64


65. Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote. 65


66. Kisha tukawazamisha hao wengine. 66


67. Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini. 67


68. Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 68


69. Na wasomee khabari za Ibrahim. 69


70. Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini? 70


71. Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea. 71


72. Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita? 72


73. Au yanakufaeni, au yanakudhuruni? 73


74. Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo. 74


75. Je! Mmewaona hawa mnao waabudu- 75


76. Nyinyi na baba zenu wa zamani? 76


77. Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 77


78. Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa, 78


79. Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha. 79


80. Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha. 80


81. Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha. 81


82. Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo. 82


83. Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema. 83


84. Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye. 84


85. Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema. 85


86. Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu. 86


87. Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa. 87


88. Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana. 88


89. Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi. 89


90. Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu. 90


91. Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu. 91


92. Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu 92


93. Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe? 93


94. Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu, 94


95. Na majeshi ya Ibilisi yote. 95


96. Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo: 96


97. Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri, 97


98. Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote. 98


99. Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote. 99


100. Basi hatuna waombezi. 100


101. Wala rafiki wa dhati. 101


102. Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini. 102


103. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini. 103


104. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 104


105. Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume. 105


106. Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu? 106


107. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. 107


108. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. 108


109. Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 109


110. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. 110


111. Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini? 111


112. Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya? 112


126. Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua! 113


114. Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini. 114


115. Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri. 115


116. Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe. 116


117. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha. 117


118. Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini. 118


119. Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni. 119


120. Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia. 120


121. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 121


122. Kina A'd waliwakanusha Mitume. 122


123. Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu? 123


124. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. 124


125. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. 125


126. Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 126


127. Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi? 127


128. Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele! 128


129. Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari. 129


130. Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari. 130


131. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini. 131


132. Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua. 132


133. Amekupeni wanyama wa kufuga na wana. 133


134. Na mabustani na chemchem. 134


135. Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa. 135


136. Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha. 136


137. Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani. 137


138. Wala sisi hatutaadhibiwa. 138


139. Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini. 139


140. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 140


141. Kina Thamud waliwakanusha Mitume. 141


142. Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu? 142


143. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. 143


144. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini. 144


145. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 145


146. Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa? 146


147. Katika mabustani, na chemchem? 147


148. Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva. 148


149. Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi. 149


150. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. 150


151. Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka, 151


152. Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi. 152


153. Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa. 153


154. Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli. 154


155. Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu. 155


156. Wala ms!imguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa. 156


157. Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta. 157


158. Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini. 158


159. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 159


160. Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume. 160


161. Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu? 161


162. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu. 162


163. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi. 163


164. Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 164


165. Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume? 165


166. Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka! 166


167. Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji! 167


168. Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu. 168


169. Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo. 169


170. Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote, 170


171. Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma. 171


172. Kisha tukawaangamiza wale wengine. 172


173. Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa. 173


174. Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini. 174


175. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. 175


176. Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume. 176


177. Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu? 177


178. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. 178


179. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. 179


180. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 180


181. Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja. 181


182. Na pimeni kwa haki iliyo nyooka; 182


183. Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi. 183


184. Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia. 184


185. Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa. 185


186. Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo. 186


187. Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli. 187


188. Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda. 188


189. Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa. 189


190. Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini. 190


191. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 191


192. Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote. 192


193. Ameuteremsha Roho muaminifu, 193


194. Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji, 194


195. Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi. 195


196. Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale. 196


197. Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili? 197


198. Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu, 198


199. Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini. 1990


200. Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu. 200


201. Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu. 201


202. Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari. 202


203. Na watasema: Je, tutapewa muhula? 203


204. Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu? 204


205. Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka, 205


206. Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa, 206


207. Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa? 207


208. Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji 208


209. Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu. 209


210. Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo, 10


211. Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi. 11


212. Hakika hao wametengwa na kusikia. 12


213. Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa. 13


214. Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe. 14


215. Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini. 15


216. Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda. 16


217. Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. 17


218. Ambaye anakuona unapo simama, 18


219. Na mageuko yako kati ya wanao sujudu. 19


220. Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua. 20


221. Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani? 21


222. Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi. 22


223. Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo. 23


224. Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata. 24


225. Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde? 25


226. Na kwamba wao husema wasiyo yatenda? 26


227. Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka. 27


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani