Al Qadr maelezo
Kwa jina la Mwenyeezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu
Utangulizi:
Rudi kwenye sura
* 1. Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika usiku wa Cheo na Utukufu.
Rudi kwenye sura
* 2. Na kitu gani kitakufunza ni nini usiku huo wa Cheo na Utukufu?
Rudi kwenye sura
* 3. Usiku wa Qadr na Sharaf, Cheo na Utukufu, ni bora kuliko miezi elfu, kwa
kuwa umekhusika kwa kuteremka ndani yake Qur'ani tukufu.
Rudi kwenye sura
* 4. Huteremka Malaika na Jibrili katika usiku huo mpaka kwenye ardhi kwa idhini
ya Mola wao Mlezi kwa sababu ya kila jambo.
Rudi kwenye sura
* 5. Na wameaminika na maudhi na uovu. Hali inabaki hivyo mpaka mapambazuko ya alfajiri.
Rudi kwenye sura
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani