| 101.Surat Al-Qaaria'h |
| Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
| Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Inayo gonga!
1

2. Nini Inayo gonga?
2

3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
3

4. Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
4

5. Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
5

6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
6

7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
7

8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
8

9. Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
9

10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
10

11. Ni Moto mkali!
11
| Sura Nyingine | Faharasa |