Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
101.Surat Al-Qaaria'h

Imeshuka Makka Ina aya 11
Utangulizi Orodha ya Sura Faharasa


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0



1. Inayo gonga! 1



2. Nini Inayo gonga? 2



3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? 3



4. Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; 4



5. Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! 5



6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, 6



7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. 7



8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, 8



9. Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! 9



10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? 10



11. Ni Moto mkali! 11


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani