Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
104.Surat Al-Humazah

Imeshuka Makka Ina aya 9
Utangulizi Sura Nyingine Faharasa


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0



1. Ole wake kila safihi, msengenyaji! 1



2. Aliye kusanya mali na kuyahisabu. 2



3. Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! 3



4. Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. 4



5. Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? 5



6. Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. 6



7. Ambao unapanda nyoyoni. 7



8. Hakika huo utafungiwa nao 8



9. Kwenye nguzo zilio nyooshwa. 9


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani