| 105.Surat Al-Fiil |
| Imeshuka Makka | Ina aya 5 |
| Utangulizi | Sura Nyingine | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye
tembo?
1

2. Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
2

3. Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
3

4. Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
4

5. Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
5
| Sura Nyingine | Faharasa |