| 107.Surat Al-Maau'n |
| Imeshuka Makka | Ina aya 7 |
| Utangulizi | Sura Nyingine | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?
1

2. Huyo ndiye anaye msukuma yatima,
2

3. Wala hahimizi kumlisha masikini.
3

4. Basi, ole wao wanao sali,
4

5. Ambao wanapuuza Sala zao;
5

6. Ambao wanajionyesha,
6

7. Nao huku wanazuia msaada.
7
| Sura Nyingine | Faharasa |