93.Surat Wadh-Dhuhaa |
Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0
1. Naapa kwa mchana!
1
2. Na kwa usiku unapo tanda!
2
3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
3
4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
4
5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
5
6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
6
7. Na akakukuta umepotea akakuongoa?
1
8. Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
8
9. Basi yatima usimwonee!
9
10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
10
11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
11
Sura Nyingine | Faharasa |