| 93.Surat Wadh-Dhuhaa |
| Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
| Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Naapa kwa mchana!
1

2. Na kwa usiku unapo tanda!
2

3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
3

4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
4

5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
5

6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
6

7. Na akakukuta umepotea akakuongoa?
1

8. Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
8

9. Basi yatima usimwonee!
9

10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
10

11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
11
| Sura Nyingine | Faharasa |