| 95.Surat At-Tin |
| Imeshuka Makka | Ina aya 8 |
| Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Naapa kwa tini na zaituni!
1

2. Na kwa Mlima wa Sinai!
2

3. Na kwa mji huu wenye amani!
3

4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
4

5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
5

6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira
usio kwisha.
6

7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
7

8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?
8
| Sura Nyingine | Faharasa |