Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili
95.Surat At-Tin

Imeshuka Makka Ina aya 8
Utangulizi Orodha ya Sura Faharasa


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0



1. Naapa kwa tini na zaituni! 1



2. Na kwa Mlima wa Sinai! 2



3. Na kwa mji huu wenye amani! 3



4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. 4



5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini! 5



6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. 6



7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? 7



8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote? 8


Sura Nyingine Faharasa

Chagua Sura Nyingine:

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani