| 99.Surat Az-Zilzalah |
| Imeshuka Madina | Ina aya 8 |
| Utangulizi | Sura Nyingine | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
1

2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
2

3. Na mtu akasema: Ina nini?
3

4. Siku hiyo itahadithia khabari zake.
4

5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!

6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
6

7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
7

8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
8
| Sura Nyingine | Faharasa |