Kwa jina la Mwenyeezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu
Maelezo: Suuratul Kaafirun

Utangulizi:

Rudi kwenye sura

* 1. Ewe Muhammad! Sema: Enyi makafiri, mlio shikilia juu ya ukafiri wenu.
Rudi kwenye sura

* 2. Mimi simuabudu mnaye muabudu nyinyi badala ya Mwenyezi Mungu.
Rudi kwenye sura

* 3. Wala nyinyi si wenye kumuabudu huyo ambaye mimi namuabudu, naye ni Mwenyezi Mungu wa pekee.
Rudi kwenye sura

* 4. Wala mimi si mwenye kuabudu mfano wa ibada yenu, kwani nyinyi ni washirikina.
Rudi kwenye sura

* 5. Wala nyinyi si wenye kuabudu mfano wa ibada yangu, kwani hii ni Tawhidi, ibada ya Mungu Mmoja.
Rudi kwenye sura

* 6. Nyinyi mna dini yenu mnayo itakidi, na mimi nina Dini yangu aliyo niteulia Mwenyezi Mungu niishike.
Rudi kwenye sura

Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani