| 100.Surat Al-A'adiyaat |
| Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
| Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
1

2. Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
2

3. Wakishambulia wakati wa asubuhi,
3

4. Huku wakitimua vumbi,
4

5. Na wakijitoma kati ya kundi,
5

6. Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
6

7. Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
7

8. Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
8

9. Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
9

10. Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
10

11. Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na
khabari zao wote!
11
| Sura Nyingine | Faharasa |